-->
logo

034 - Sabaa

  سَبَاء
Sabaa: 34


بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ



الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَلَهُ الْحَمْدُ فِي الْآخِرَةِ ۚ وَهُوَ الْحَكِيمُ الْخَبِيرُ ﴿١﴾
1.  AlhamduliLLaah, Ambaye ni Vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini, na Himidi ni Zake katika Aakhirah Naye ni Mwenye hikmah wa yote, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika.



يَعْلَمُ مَا يَلِجُ فِي الْأَرْضِ وَمَا يَخْرُجُ مِنْهَا وَمَا يَنزِلُ مِنَ السَّمَاءِ وَمَا يَعْرُجُ فِيهَا ۚ وَهُوَ الرَّحِيمُ الْغَفُورُ ﴿٢﴾
2. Anajua yanayoingia ardhini, na yanayotoka humo, na yanayoteremka kutoka mbinguni, na yanayopanda huko; Naye Ndiye Mwenye kurehemu, Mwingi wa kughufuria.



وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لَا تَأْتِينَا السَّاعَةُ ۖ قُلْ بَلَىٰ وَرَبِّي لَتَأْتِيَنَّكُمْ عَالِمِ الْغَيْبِ ۖ لَا يَعْزُبُ عَنْهُ مِثْقَالُ ذَرَّةٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ وَلَا أَصْغَرُ مِن ذَٰلِكَ وَلَا أَكْبَرُ إِلَّا فِي كِتَابٍ مُّبِينٍ ﴿٣﴾
3. Na wale waliokufuru wakasema: “Saa haitotufikia!” Sema: Bali la! Naapa kwa Rabb wangu! Bila shaka itakufikieni; Mjuzi wa ghayb; hakuna kinachofichika Kwake hata chenye uzito wa chembe (au sisimizi) mbinguni wala ardhini, na wala kidogo zaidi kuliko hicho, na wala kikubwa zaidi kuliko hicho isipokuwa kimo katika Kitabu kinachobainisha.


لِّيَجْزِيَ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ ۚ أُولَـٰئِكَ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَرِزْقٌ كَرِيمٌ ﴿٤﴾
4. Ili Awalipe wale walioamini na wakatenda mema. Hao watapata maghfirah na riziki tukufu.



وَالَّذِينَ سَعَوْا فِي آيَاتِنَا مُعَاجِزِينَ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مِّن رِّجْزٍ أَلِيمٌ ﴿٥﴾
5. Na wale waliofanya bidii katika Aayaat (na ishara) Zetu watake kuzibatilisha hao watapata adhabu mbaya ya kufadhaika, iumizayo.


وَيَرَى الَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ الَّذِي أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ هُوَ الْحَقَّ وَيَهْدِي إِلَىٰ صِرَاطِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ ﴿٦﴾
6. Na wale waliopewa elimu wanaona kuwa yale yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Rabb wako ndio haki, na yanaongoza kwenye njia ya Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote.


وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا هَلْ نَدُلُّكُمْ عَلَىٰ رَجُلٍ يُنَبِّئُكُمْ إِذَا مُزِّقْتُمْ كُلَّ مُمَزَّقٍ إِنَّكُمْ لَفِي خَلْقٍ جَدِيدٍ ﴿٧﴾
7. Na wale waliokufuru wakasema: “Je, tukuelekezeni kwa mtu anayekujulisheni kwamba mtakapomomonyoka mkawa vumbi lilotawanyika mbali, mtakuwa katika umbo jipya?”



أَفْتَرَىٰ عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا أَم بِهِ جِنَّةٌ ۗ بَلِ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ فِي الْعَذَابِ وَالضَّلَالِ الْبَعِيدِ﴿٨﴾
8. “Je, amemtungia Allaah uongo, au ana wazimu?”  Bali wale wasioamini Aakhirah watakuwa katika adhabu na upotofu wa mbali.



أَفَلَمْ يَرَوْا إِلَىٰ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُم مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ ۚ إِن نَّشَأْ نَخْسِفْ بِهِمُ الْأَرْضَ أَوْ نُسْقِطْ عَلَيْهِمْ كِسَفًا مِّنَ السَّمَاءِ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لِّكُلِّ عَبْدٍ مُّنِيبٍ ﴿٩﴾
9. Je, kwani hawaoni yale yaliyoko mbele yao na yale yaliyo nyuma yao ya mbingu na ardhi? Tungelitaka, Tungeliwadidimiza ardhini, au Tungeliwaangushia juu yao vipande vya mbingu. Hakika katika hayo kuna Aayah (ishara, dalili) kwa kila mja anayerudia rudia kutubu (kwa Allaah).



وَلَقَدْ آتَيْنَا دَاوُودَ مِنَّا فَضْلًا ۖ يَا جِبَالُ أَوِّبِي مَعَهُ وَالطَّيْرَ ۖ وَأَلَنَّا لَهُ الْحَدِيدَ ﴿١٠﴾
10. Na kwa yakini Tulimpa Daawuwd fadhila kutoka Kwetu, (Tukasema): “Ee majabali! Rejesheni kumsabbih (Allaah) pamoja naye na ndege pia.” Na Tukamlainishia chuma.


أَنِ اعْمَلْ سَابِغَاتٍ وَقَدِّرْ فِي السَّرْدِ ۖ وَاعْمَلُوا صَالِحًا ۖ إِنِّي بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ ﴿١١﴾
11. Na kwamba: “Tengenezeni mavazi ya chuma mapana, na kadiria sawasawa katika kuunganisha darayana tendeni mema; hakika Mimi ni Mwenye kuona myatendayo.


وَلِسُلَيْمَانَ الرِّيحَ غُدُوُّهَا شَهْرٌ وَرَوَاحُهَا شَهْرٌ ۖ وَأَسَلْنَا لَهُ عَيْنَ الْقِطْرِ ۖ وَمِنَ الْجِنِّ مَن يَعْمَلُ بَيْنَ يَدَيْهِ بِإِذْنِ رَبِّهِ ۖ وَمَن يَزِغْ مِنْهُمْ عَنْ أَمْرِنَا نُذِقْهُ مِنْ عَذَابِ السَّعِيرِ ﴿١٢﴾
12. Na kwa Sulaymaan Tulimuitishia upepo; safari yake ya asubuhi ni mwezi, na safari yake ya jioni ni mwezi, na Tukamtiririzia chemchemu za shaba. Na miongoni mwa majini wanaofanyia kazi mbele yake kwa idhini ya Rabb wake. Na yeyote atakayezikengeuka amri Zetu, Tutamuonjesha adhabu ya moto uliowashwa vikali mno.” 


يَعْمَلُونَ لَهُ مَا يَشَاءُ مِن مَّحَارِيبَ وَتَمَاثِيلَ وَجِفَانٍ كَالْجَوَابِ وَقُدُورٍ رَّاسِيَاتٍ ۚ اعْمَلُوا آلَ دَاوُودَ شُكْرًا ۚ وَقَلِيلٌ مِّنْ عِبَادِيَ الشَّكُورُ ﴿١٣﴾
13. Wanamfanyia kazi atakayo; ngome ndefu za fakhari na masanamu, na mabakuli makubwa kama mahodhi na masufuria makubwa yaliyothibiti imara. (Tukasema): “Tendeni enyi familia ya Daawuwd kwa shukurani!” Na wachache miongoni mwa waja Wangu wenye kushukuru.



فَلَمَّا قَضَيْنَا عَلَيْهِ الْمَوْتَ مَا دَلَّهُمْ عَلَىٰ مَوْتِهِ إِلَّا دَابَّةُ الْأَرْضِ تَأْكُلُ مِنسَأَتَهُ ۖ فَلَمَّا خَرَّ تَبَيَّنَتِ الْجِنُّ أَن لَّوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ الْغَيْبَ مَا لَبِثُوا فِي الْعَذَابِ الْمُهِينِ ﴿١٤﴾
14. Basi Tulipomkidhia mauti, hakuna kilichowajulisha kifo chake isipokuwa mdudu wa ardhi akila fimbo yake. Basi alipoanguka ikawabainika majini kwamba lau wangelikuwa wanajua ya ghayb, basi wasingebakia katika adhabu ya kudhalilisha.



لَقَدْ كَانَ لِسَبَإٍ فِي مَسْكَنِهِمْ آيَةٌ ۖ جَنَّتَانِ عَن يَمِينٍ وَشِمَالٍ ۖ كُلُوا مِن رِّزْقِ رَبِّكُمْ وَاشْكُرُوا لَهُ ۚبَلْدَةٌ طَيِّبَةٌ وَرَبٌّ غَفُورٌ ﴿١٥﴾
15. Kwa yakini ilikuwa ni Aayah (ishara, dalili) kwa kina Sabaa katika masikani zao. Bustani mbili; kulia na kushoto. (Wakaambiwa): “Kuleni katika riziki ya Rabb wenu na mshukuruni. Mji mzuri na Rabb Ambaye ni Mwingi wa kughufuria.



فَأَعْرَضُوا فَأَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ سَيْلَ الْعَرِمِ وَبَدَّلْنَاهُم بِجَنَّتَيْهِمْ جَنَّتَيْنِ ذَوَاتَيْ أُكُلٍ خَمْطٍ وَأَثْلٍ وَشَيْءٍ مِّن سِدْرٍ قَلِيلٍ ﴿١٦﴾
16. Lakini wakakengeuka, basi Tukawapelekea mafuriko ya mabwawa, na Tukawabadilishia badala ya bustani zao mbili kwa bustani mbili nyinginezo zenye matunda machungu mno na mivinje na baadhi ya mikunazi kidogo. 



ذَٰلِكَ جَزَيْنَاهُم بِمَا كَفَرُوا ۖ وَهَلْ نُجَازِي إِلَّا الْكَفُورَ ﴿١٧﴾
17. Hivyo ndivyo Tulivyowalipa kwa vile walivyokufuru. Na Hatuadhibu isipokuwa anayekufuru.



وَجَعَلْنَا بَيْنَهُمْ وَبَيْنَ الْقُرَى الَّتِي بَارَكْنَا فِيهَا قُرًى ظَاهِرَةً وَقَدَّرْنَا فِيهَا السَّيْرَ ۖ سِيرُوا فِيهَا لَيَالِيَ وَأَيَّامًا آمِنِينَ ﴿١٨﴾
18. Na Tukaweka baina yao na baina ya miji Tuliyoibariki; miji mingine iliyodhihirika, na Tukakadiria humo vituo vya safari. (Tukasema): “Safirini humo usiku na mchana kwa amani.”



فَقَالُوا رَبَّنَا بَاعِدْ بَيْنَ أَسْفَارِنَا وَظَلَمُوا أَنفُسَهُمْ فَجَعَلْنَاهُمْ أَحَادِيثَ وَمَزَّقْنَاهُمْ كُلَّ مُمَزَّقٍ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّكُلِّ صَبَّارٍ شَكُورٍ ﴿١٩﴾
19. Wakasema: “Rabb wetu! Baidisha baina ya safari zetu.” Na wakazidhulumu nafsi zao; Tukawafanya kuwa ni simulizi, Tukawafarikisha na kuwatawanyatawanya barabara. Hakika katika hayo bila shaka (kuna) Aayaat (zingatio, ishara) kwa kila mwingi wa kushukuru na mwingi wa kusubiri.


وَلَقَدْ صَدَّقَ عَلَيْهِمْ إِبْلِيسُ ظَنَّهُ فَاتَّبَعُوهُ إِلَّا فَرِيقًا مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٢٠﴾
20. Na kwa yakini Ibliys alisadikisha dhana yake juu yao, basi walimfuata isipokuwa kundi miongoni mwa Waumini.



وَمَا كَانَ لَهُ عَلَيْهِم مِّن سُلْطَانٍ إِلَّا لِنَعْلَمَ مَن يُؤْمِنُ بِالْآخِرَةِ مِمَّنْ هُوَ مِنْهَا فِي شَكٍّ ۗ وَرَبُّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ حَفِيظٌ ﴿٢١﴾
21. Na yeye (Ibliys) hakuwa ana madaraka yoyote juu yao isipokuwa ili Tujue ni nani yule anayeamini Aakhirah na nani yule anayeitilia shaka. Na Rabb wako ni Mwenye kuhifadhi kitu.



قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِ اللَّـهِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ وَمَا لَهُمْ فِيهِمَا مِن شِرْكٍ وَمَا لَهُ مِنْهُم مِّن ظَهِيرٍ ﴿٢٢﴾
22. Sema: “Ombeni wale mnaodai kwa dhana (ni waabudiwa) badala ya Allaah, hawamiliki hata uzito wa sisimizi mbinguni wala ardhini, na wala hawana humo ushirika Naye, na wala Yeye (Allaah) Hana msaidizi miongoni mwao.”



وَلَا تَنفَعُ الشَّفَاعَةُ عِندَهُ إِلَّا لِمَنْ أَذِنَ لَهُ ۚ حَتَّىٰ إِذَا فُزِّعَ عَن قُلُوبِهِمْ قَالُوا مَاذَا قَالَ رَبُّكُمْ ۖ قَالُوا الْحَقَّ ۖ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْكَبِيرُ ﴿٢٣﴾
23. Na wala haitofaa ash-shafaa’ah (uombezi) mbele Yake isipokuwa kwa yule Aliyempa idhini, mpaka itakapoondolewa fazaiko nyoyoni mwao; watasema: “Amesema nini Rabb wenu?” Watasema: “Ya haki”; Naye ni Mwenye ‘Uluwa, Ametukuka, Mkubwa wa dhati vitendo na sifa.



قُلْ مَن يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ قُلِ اللَّـهُ ۖ وَإِنَّا أَوْ إِيَّاكُمْ لَعَلَىٰ هُدًى أَوْ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٢٤﴾
24. Sema: “Nani yule anayekuruzukuni kutoka mbinguni na ardhini?”  Sema: “Ni Allaah!  Na hakika ima sisi au nyinyi, bila shaka tuko juu ya Uongofu au katika upotofu bayana.”


قُل لَّا تُسْأَلُونَ عَمَّا أَجْرَمْنَا وَلَا نُسْأَلُ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٢٥﴾
25. Sema: “Hamtoulizwa kuhusu ule uhalifu tulioufanya, na wala hatutoulizwa kwa yale mnayoyatenda.”


قُلْ يَجْمَعُ بَيْنَنَا رَبُّنَا ثُمَّ يَفْتَحُ بَيْنَنَا بِالْحَقِّ وَهُوَ الْفَتَّاحُ الْعَلِيمُ ﴿٢٦﴾
26. Sema: “Rabb wetu Atatukusanya, kisha Atahukumu baina yetu kwa haki, Naye Ndiye Hakimu, Mjuzi wa yote.


قُلْ أَرُونِيَ الَّذِينَ أَلْحَقْتُم بِهِ شُرَكَاءَ ۖ كَلَّا ۚ بَلْ هُوَ اللَّـهُ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٢٧﴾
27. Sema: “Nionyesheni wale mliowaunganisha Naye kuwa washirika. Laa hasha! Bali Yeye Ndiye Allaah Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika,  Mwenye hikmah wa yote.


وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا كَافَّةً لِّلنَّاسِ بَشِيرًا وَنَذِيرًا وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٢٨﴾
28. Na Hatukukutuma (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) isipokuwa kwa watu wote uwe mbashiriaji na muonyaji, lakini watu wengi hawajui.


وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَـٰذَا الْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٢٩﴾
29. Na wanasema: “Ni lini hiyo ahadi (ya Qiyaamah), mkiwa ni wasemao kweli?”


قُل لَّكُم مِّيعَادُ يَوْمٍ لَّا تَسْتَأْخِرُونَ عَنْهُ سَاعَةً وَلَا تَسْتَقْدِمُونَ ﴿٣٠﴾
30. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Mnayo miadi Siku ambayo hamtoiakhirisha saa, na wala hamtakadimisha.”



وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لَن نُّؤْمِنَ بِهَـٰذَا الْقُرْآنِ وَلَا بِالَّذِي بَيْنَ يَدَيْهِ ۗ وَلَوْ تَرَىٰ إِذِ الظَّالِمُونَ مَوْقُوفُونَ عِندَ رَبِّهِمْ يَرْجِعُ بَعْضُهُمْ إِلَىٰ بَعْضٍ الْقَوْلَ يَقُولُ الَّذِينَ اسْتُضْعِفُوا لِلَّذِينَ اسْتَكْبَرُوا لَوْلَا أَنتُمْ لَكُنَّا مُؤْمِنِينَ ﴿٣١﴾
31. Na wale waliokufuru wakasema: “Hatutoiamini Qur-aan hii, na wala yale yaliyokuwa kabla yake.” Na lau ungeliona madhalimu pale watakaposimamishwa mbele ya Rabb wao, wakirejesheana wenyewe kwa wenyewe maneno; watasema wale waliodhoofishwa kuwaambia wale waliotakabari: “Lau ingelikuwa si nyinyi, bila shaka tungelikuwa Waumini.”



قَالَ الَّذِينَ اسْتَكْبَرُوا لِلَّذِينَ اسْتُضْعِفُوا أَنَحْنُ صَدَدْنَاكُمْ عَنِ الْهُدَىٰ بَعْدَ إِذْ جَاءَكُم ۖ بَلْ كُنتُم مُّجْرِمِينَ ﴿٣٢﴾
32. Na watasema wale waliotakabari kuwaambia wale waliodhoofishwa: “Je, kwani sisi ndio tuliokuzuieni na Mwongozo baada ya kukujieni? Bali nyinyi mlikuwa wahalifu.”



وَقَالَ الَّذِينَ اسْتُضْعِفُوا لِلَّذِينَ اسْتَكْبَرُوا بَلْ مَكْرُ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ إِذْ تَأْمُرُونَنَا أَن نَّكْفُرَ بِاللَّـهِ وَنَجْعَلَ لَهُ أَندَادًا ۚ وَأَسَرُّوا النَّدَامَةَ لَمَّا رَأَوُا الْعَذَابَ وَجَعَلْنَا الْأَغْلَالَ فِي أَعْنَاقِ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚهَلْ يُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٣٣﴾
33. Na watasema waliodhoofishwa kuwaambia wale waliotakabari: “Bali ni njama (zenu) za usiku na mchana, mlipotuamrisha tumkufuru Allaah na Tumfanyie wa kumsawazisha Naye.” Na wataficha au watadhihirisha majuto watakapoiona adhabu. Na Tutajaalia minyororo shingoni mwa wale waliokufuru. Je, wanalipwa isipokuwa yale waliyokuwa wakiyatenda?”


وَمَا أَرْسَلْنَا فِي قَرْيَةٍ مِّن نَّذِيرٍ إِلَّا قَالَ مُتْرَفُوهَا إِنَّا بِمَا أُرْسِلْتُم بِهِ كَافِرُونَ ﴿٣٤﴾
34. Na Hatukupeleka katika mji wowote ule mwonyaji yeyote isipokuwa wamesema wastareheshwa wake kwa anasa za dunia: “Hakika sisi kwa yale mliotumwa nayo ni wenye kuyakanusha.”


وَقَالُوا نَحْنُ أَكْثَرُ أَمْوَالًا وَأَوْلَادًا وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ ﴿٣٥﴾
35. Na wakasema: “Sisi tuna mali nyingi zaidi na auladi na hivyo sisi hatutaadhibiwa.”



قُلْ إِنَّ رَبِّي يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ وَيَقْدِرُ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٣٦﴾
36. Sema: “Hakika Rabb wangu Anamkunjulia riziki kwa Amtakaye, na Anabana, lakini watu wengi hawajui.”



وَمَا أَمْوَالُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُم بِالَّتِي تُقَرِّبُكُمْ عِندَنَا زُلْفَىٰ إِلَّا مَنْ آمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا فَأُولَـٰئِكَ لَهُمْ جَزَاءُ الضِّعْفِ بِمَا عَمِلُوا وَهُمْ فِي الْغُرُفَاتِ آمِنُونَ ﴿٣٧﴾
37. Na si mali zenu na wala watoto wenu ambavyo vitakukurubisheni Kwetu muwe karibu isipokuwa yule aliyeamini na akatenda mema, basi hao watapata malipo maradufu kutokana na yale waliyoyatenda, nao watakuwa katika maghorofa (Jannah) wenye amani.


وَالَّذِينَ يَسْعَوْنَ فِي آيَاتِنَا مُعَاجِزِينَ أُولَـٰئِكَ فِي الْعَذَابِ مُحْضَرُونَ ﴿٣٨﴾
38. Na wale wanaofanya bidii katika Aayaat (na ishara, hoja) Zetu watake wazibatilishe, hao watahudhurishwa kwenye adhabu.



قُلْ إِنَّ رَبِّي يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ وَيَقْدِرُ لَهُ ۚ وَمَا أَنفَقْتُم مِّن شَيْءٍ فَهُوَ يُخْلِفُهُ ۖ وَهُوَ خَيْرُ الرَّازِقِينَ ﴿٣٩﴾
39. Sema: “Hakika Rabb wangu Anakunjua riziki kwa Amtakaye kati ya waja Wake, na Anambania. Na kitu chochote mtoacho, basi Yeye Atakilipa, Naye ni Mbora wa wenye kuruzuku.



وَيَوْمَ يَحْشُرُهُمْ جَمِيعًا ثُمَّ يَقُولُ لِلْمَلَائِكَةِ أَهَـٰؤُلَاءِ إِيَّاكُمْ كَانُوا يَعْبُدُونَ ﴿٤٠﴾
40. Na Siku Atakayowakusanya wote, kisha Atawaambia Malaika: “Je, hawa  ndio waliokuwa wakikuabuduni?”  


قَالُوا سُبْحَانَكَ أَنتَ وَلِيُّنَا مِن دُونِهِم ۖ بَلْ كَانُوا يَعْبُدُونَ الْجِنَّ ۖ أَكْثَرُهُم بِهِم مُّؤْمِنُونَ ﴿٤١﴾
41. Watasema: “Subhaanak! Utakasifu ni Wako Wewe ni Mlinzi, Msaidizi wetu, sio hao!” Bali walikuwa wakiabudu majini, wengi wao wakiwaamini.



فَالْيَوْمَ لَا يَمْلِكُ بَعْضُكُمْ لِبَعْضٍ نَّفْعًا وَلَا ضَرًّا وَنَقُولُ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا ذُوقُوا عَذَابَ النَّارِ الَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ ﴿٤٢﴾
42. Basi leo hawatoweza baadhi yenu kuwapatia wenziwenu manufaa yoyote na wala madhara yoyote, na Tutawaambia wale waliodhulumu: “Onjeni adhabu ya moto ambao mlikuwa mkiukadhibisha.”



وَإِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ آيَاتُنَا بَيِّنَاتٍ قَالُوا مَا هَـٰذَا إِلَّا رَجُلٌ يُرِيدُ أَن يَصُدَّكُمْ عَمَّا كَانَ يَعْبُدُ آبَاؤُكُمْ وَقَالُوا مَا هَـٰذَا إِلَّا إِفْكٌ مُّفْتَرًى ۚ وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلْحَقِّ لَمَّا جَاءَهُمْ إِنْ هَـٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ﴿٤٣﴾
43. Na wanaposomewa Aayaat Zetu bayana, husema: “Huyu (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) si chochote isipokuwa mtu anataka akuzuieni na yale waliyokuwa wakiyaabudu baba zenu.” Na husema: “Hii (Qur-aan) si chochote isipokuwa uzushi uliotungwa.” Na wale waliokufuru wakasema kuhusu haki ilipowajia: “Hii si chochote isipokua ni sihiri bayana.”


وَمَا آتَيْنَاهُم مِّن كُتُبٍ يَدْرُسُونَهَا ۖ وَمَا أَرْسَلْنَا إِلَيْهِمْ قَبْلَكَ مِن نَّذِيرٍ ﴿٤٤﴾
44. Na wala Hatukuwapa kitabu chochote wakisomacho, na wala Hatukuwapelekea kabla yako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) mwonyaji yeyote.


وَكَذَّبَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ وَمَا بَلَغُوا مِعْشَارَ مَا آتَيْنَاهُمْ فَكَذَّبُوا رُسُلِي ۖ فَكَيْفَ كَانَ نَكِيرِ ﴿٤٥﴾
45. Na walikadhibisha wale wa kabla yao, na (hawa Maquraysh) hawakufikia sehemu moja ya kumi katika yale Tuliyowapa kisha wakakadhibisha Rusuli Wangu; basi ilikuwa vipi kukana Kwangu. 



قُلْ إِنَّمَا أَعِظُكُم بِوَاحِدَةٍ ۖ أَن تَقُومُوا لِلَّـهِ مَثْنَىٰ وَفُرَادَىٰ ثُمَّ تَتَفَكَّرُوا ۚ مَا بِصَاحِبِكُم مِّن جِنَّةٍ ۚ إِنْ هُوَ إِلَّا نَذِيرٌ لَّكُم بَيْنَ يَدَيْ عَذَابٍ شَدِيدٍ ﴿٤٦﴾
46. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika nakuwaidhini kwa jambo moja tu!  Msimame kwa ajili ya Allaah wawili wawili, au mmoja mmoja kisha mtafakari.” Sahibu yenu si mwendawazimu. Yeye si chochote isipokuwa mwonyaji kwenu, kabla ya kufikia adhabu kali.



قُلْ مَا سَأَلْتُكُم مِّنْ أَجْرٍ فَهُوَ لَكُمْ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَى اللَّـهِ ۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ ﴿٤٧﴾
47. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Ujira wowote kama nimekuombeni basi huo ni wenu; sina ujira ila kwa Allaah tu. Naye juu ya kila kitu ni Shahidi.


قُلْ إِنَّ رَبِّي يَقْذِفُ بِالْحَقِّ عَلَّامُ الْغُيُوبِ ﴿٤٨﴾
48. Sema: “Hakika Rabb wangu Anateremsha haki, ni Mjuzi wa ghayb. 



قُلْ جَاءَ الْحَقُّ وَمَا يُبْدِئُ الْبَاطِلُ وَمَا يُعِيدُ ﴿٤٩﴾
49. Sema: “Haki imekuja, na ubatilifu hauchomozi, na wala haurudi.”



قُلْ إِن ضَلَلْتُ فَإِنَّمَا أَضِلُّ عَلَىٰ نَفْسِي ۖ وَإِنِ اهْتَدَيْتُ فَبِمَا يُوحِي إِلَيَّ رَبِّي ۚ إِنَّهُ سَمِيعٌ قَرِيبٌ﴿٥٠﴾
50. Sema: “Ikiwa nimepotoka, basi hakika nimepotoka kwa khasara ya nafsi yangu, na ikiwa nimeongoka, basi ni kwa yale Aliyonifunulia Wahy Rabb wangu; hakika Yeye ni Mwenye kusikia yote, Yu karibu kwa elimu Yake.”


وَلَوْ تَرَىٰ إِذْ فَزِعُوا فَلَا فَوْتَ وَأُخِذُوا مِن مَّكَانٍ قَرِيبٍ ﴿٥١﴾
51. Na lau ungeliona watakapofazaika kwa khofu, basi hakuna kukwepa, na watachukuliwa kutoka mahali pa karibu.


وَقَالُوا آمَنَّا بِهِ وَأَنَّىٰ لَهُمُ التَّنَاوُشُ مِن مَّكَانٍ بَعِيدٍ ﴿٥٢﴾
52. Na watasema: “(Sasa) Tumemwamini Allaah!” Lakini wataweza wapi kuipata (iymaan) kutoka mahali mbali?


وَقَدْ كَفَرُوا بِهِ مِن قَبْلُ ۖ وَيَقْذِفُونَ بِالْغَيْبِ مِن مَّكَانٍ بَعِيدٍ ﴿٥٣﴾
53. Na kwa yakini walikwishaikanusha kabla, na wanavurumisha ghayb kwa dhana kutoka mahali mbali.


وَحِيلَ بَيْنَهُمْ وَبَيْنَ مَا يَشْتَهُونَ كَمَا فُعِلَ بِأَشْيَاعِهِم مِّن قَبْلُ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا فِي شَكٍّ مُّرِيبٍ ﴿٥٤﴾
54. Na kizuizi kitawekwa baina yao na baina yale wanayoyatamani, kama walivyofanyiwa wenzao kabla. Hakika wao walikuwa katika shaka yenye kutia wasiwasi. 



Tags

advertisement centil

This blog is created for your interest and in our interest as well as a website and social media sharing info Interest and Other Entertainment.