-->
logo

038 - Swaad

ص
Swaad:  38

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ


ص ۚ وَالْقُرْآنِ ذِي الذِّكْرِ ﴿١﴾
1.  Swaad. Naapa kwa Qur-aan iliyojaa ukumbusho na taadhima.


بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي عِزَّةٍ وَشِقَاقٍ ﴿٢﴾
2. Bali wale waliokufuru wamo katika majivuno na upinzani.


كَمْ أَهْلَكْنَا مِن قَبْلِهِم مِّن قَرْنٍ فَنَادَوا وَّلَاتَ حِينَ مَنَاصٍ ﴿٣﴾
3. Karne ngapi Tumeangamiza kabla yao wakaomba uokozi  lakini hakukuwa tena na wakati wa kuokoka.


وَعَجِبُوا أَن جَاءَهُم مُّنذِرٌ مِّنْهُمْ ۖ وَقَالَ الْكَافِرُونَ هَـٰذَا سَاحِرٌ كَذَّابٌ ﴿٤﴾
4. Na wakastaajabu kwamba amewajia mwonyaji miongoni mwao, na wakasema makafiri: “Huyu ni mchawi muongo.”


أَجَعَلَ الْآلِهَةَ إِلَـٰهًا وَاحِدًا ۖ إِنَّ هَـٰذَا لَشَيْءٌ عُجَابٌ ﴿٥﴾
5. “Amewafanya waabudiwa kuwa ni Ilaah Mmoja?  Hakika hili ni jambo la ajabu mno!”



وَانطَلَقَ الْمَلَأُ مِنْهُمْ أَنِ امْشُوا وَاصْبِرُوا عَلَىٰ آلِهَتِكُمْ ۖ إِنَّ هَـٰذَا لَشَيْءٌ يُرَادُ ﴿٦﴾
6. Na wakaondoka wakuu miongoni mwao kwamba: “Nendeni zenu na subirini juu ya waabudiwa wenu, hakika hili ni jambo linalokusudiwa.


مَا سَمِعْنَا بِهَـٰذَا فِي الْمِلَّةِ الْآخِرَةِ إِنْ هَـٰذَا إِلَّا اخْتِلَاقٌ ﴿٧﴾
7. “Hatukusikia haya katika mila ya mwisho, haya si chochote isipokuwa ni jambo lilozushwa tu.


أَأُنزِلَ عَلَيْهِ الذِّكْرُ مِن بَيْنِنَا ۚ بَلْ هُمْ فِي شَكٍّ مِّن ذِكْرِي ۖ بَل لَّمَّا يَذُوقُوا عَذَابِ ﴿٨﴾
8. “Eti ameteremshiwa ukumbusho yeye pekee miongoni mwetu?” Hapana! Wao wamo katika shaka na ukumbusho Wangu, bali hawakuonja bado adhabu Yangu.



أَمْ عِندَهُمْ خَزَائِنُ رَحْمَةِ رَبِّكَ الْعَزِيزِ الْوَهَّابِ ﴿٩﴾
9. Au wanazo hazina za rahmah za Rabb wako Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwingi wa kutunuku?


أَمْ لَهُم مُّلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ فَلْيَرْتَقُوا فِي الْأَسْبَابِ ﴿١٠﴾
10. Au wana ufalme wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake? Basi na wapande (huko) katika njia.


جُندٌ مَّا هُنَالِكَ مَهْزُومٌ مِّنَ الْأَحْزَابِ ﴿١١﴾
11. (Wao ni) vijiaskari watakaoshindwa huko katika makundi.


كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ وَعَادٌ وَفِرْعَوْنُ ذُو الْأَوْتَادِ ﴿١٢﴾
12. Walikadhibisha kabla yao watu wa Nuwh, na kina ‘Aad, na Fir’awn mwenye vigingi. 


وَثَمُودُ وَقَوْمُ لُوطٍ وَأَصْحَابُ الْأَيْكَةِ ۚ أُولَـٰئِكَ الْأَحْزَابُ ﴿١٣﴾
13. Na kina Thamuwd na watu wa Luwtw, na watu wa kichakani, hayo ndio makundi


إِن كُلٌّ إِلَّا كَذَّبَ الرُّسُلَ فَحَقَّ عِقَابِ ﴿١٤﴾
14. Hakuna hata mmoja wao isipokuwa waliwakadhibisha Rusuli, basi ikahakikika ikabu Yangu.


وَمَا يَنظُرُ هَـٰؤُلَاءِ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً مَّا لَهَا مِن فَوَاقٍ ﴿١٥﴾
15. Na hawangojei hawa isipokuwa ukelele angamizi mmoja tu usiokuwa na kurudishwa wala taakhira.


وَقَالُوا رَبَّنَا عَجِّل لَّنَا قِطَّنَا قَبْلَ يَوْمِ الْحِسَابِ ﴿١٦﴾
16. Na wanasema: “Rabb wetu! Tuharakizie fungu letu (la adhabu) kabla ya Siku ya hesabu.”



اصْبِرْ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَاذْكُرْ عَبْدَنَا دَاوُودَ ذَا الْأَيْدِ ۖ إِنَّهُ أَوَّابٌ ﴿١٧﴾
17. Subiri kwa yale wanayoyasema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم); na taja mja Wetu Daawuwd mwenye nguvu, hakika yeye ni mwenye kurudia rudia kutubia.


إِنَّا سَخَّرْنَا الْجِبَالَ مَعَهُ يُسَبِّحْنَ بِالْعَشِيِّ وَالْإِشْرَاقِ ﴿١٨﴾
18. Hakika Sisi Tulitiisha majabali yawe pamoja naye yakisabbih jioni na baada ya kuchomoza jua.


وَالطَّيْرَ مَحْشُورَةً ۖ كُلٌّ لَّهُ أَوَّابٌ ﴿١٩﴾
19. Na ndege waliokusanywa; wote walikuwa ni watiifu mno kwake.  


وَشَدَدْنَا مُلْكَهُ وَآتَيْنَاهُ الْحِكْمَةَ وَفَصْلَ الْخِطَابِ ﴿٢٠﴾
20. Na Tukamtilia nguvu ufalme wake, na Tukampa hikmah, na umaizi wa kukata hukumu.


وَهَلْ أَتَاكَ نَبَأُ الْخَصْمِ إِذْ تَسَوَّرُوا الْمِحْرَابَ ﴿٢١﴾
21. Na je, imekujia habari za wenye kukhasimiana waliporuka ukuta kuingia chumba cha kuswalia.



إِذْ دَخَلُوا عَلَىٰ دَاوُودَ فَفَزِعَ مِنْهُمْ ۖ قَالُوا لَا تَخَفْ ۖ خَصْمَانِ بَغَىٰ بَعْضُنَا عَلَىٰ بَعْضٍ فَاحْكُم بَيْنَنَا بِالْحَقِّ وَلَا تُشْطِطْ وَاهْدِنَا إِلَىٰ سَوَاءِ الصِّرَاطِ ﴿٢٢﴾
22. Walipomuingilia Daawuwd akafazaika kutokana nao! Wakasema: “Usikhofu!  (Sisi ni) makhasimu wawili; mmoja wetu amemkandamiza mwenziwe, basi hukumu baina yetu kwa haki, na wala usipendelee, na tuongoze katika njia ya sawa.


إِنَّ هَـٰذَا أَخِي لَهُ تِسْعٌ وَتِسْعُونَ نَعْجَةً وَلِيَ نَعْجَةٌ وَاحِدَةٌ فَقَالَ أَكْفِلْنِيهَا وَعَزَّنِي فِي الْخِطَابِ﴿٢٣﴾
23. “Hakika huyu ndugu yangu ana kondoo majike tisiini na tisa, nami nina kondoo jike mmoja; basi akasema: “Nikabidhi huyo awe katika amana yangu” na amenishinda kwa maneno.” 


قَالَ لَقَدْ ظَلَمَكَ بِسُؤَالِ نَعْجَتِكَ إِلَىٰ نِعَاجِهِ ۖ وَإِنَّ كَثِيرًا مِّنَ الْخُلَطَاءِ لَيَبْغِي بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَقَلِيلٌ مَّا هُمْ ۗ وَظَنَّ دَاوُودُ أَنَّمَا فَتَنَّاهُ فَاسْتَغْفَرَ رَبَّهُ وَخَرَّ رَاكِعًا وَأَنَابَ ۩﴿٢٤﴾
24. (Nabiy Daawuwd) Akasema: “Kweli amekudhulumu kwa kukuomba kondoo wako kuongezea kondoo wake. Na hakika washirika wengi hukandamizana wao kwa wao isipokuwa wale walioamini na wakatenda mema, na hao ni wachache.” Daawuwd akahisi kwamba Tumemtia mtihanini, basi akamwomba Rabb wake maghfirah na akaporomoka kusujudu na akarudi kutubia.


فَغَفَرْنَا لَهُ ذَٰلِكَ ۖ وَإِنَّ لَهُ عِندَنَا لَزُلْفَىٰ وَحُسْنَ مَآبٍ ﴿٢٥﴾
25. Tukamghufuria hayo, na hakika yeye bila shaka ana Kwetu makurubisho na marejeo mazuri.


يَا دَاوُودُ إِنَّا جَعَلْنَاكَ خَلِيفَةً فِي الْأَرْضِ فَاحْكُم بَيْنَ النَّاسِ بِالْحَقِّ وَلَا تَتَّبِعِ الْهَوَىٰ فَيُضِلَّكَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ ۚ إِنَّ الَّذِينَ يَضِلُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ لَهُمْ عَذَابٌ شَدِيدٌ بِمَا نَسُوا يَوْمَ الْحِسَابِ ﴿٢٦﴾
26.  “Ee Daawuwd!  Hakika Tumekujaalia uwe Khalifa katika ardhi. Basi hukumu baina ya watu kwa haki, na wala usifuate matamanio yakakupoteza na njia ya Allaah. Hakika wale wanaopotea njia ya Allaah watapata adhabu kali kwa sababu ya kusahau kwao Siku ya hesabu.


وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاءَ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا بَاطِلًا ۚ ذَٰلِكَ ظَنُّ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚ فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِنَ النَّارِ ﴿٢٧﴾
27. Na wala Hatukuumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yake bila kusudio. Hiyo ndio dhana ya wale waliokufuru. Basi ole wale waliokufuru kwa moto utakaowapata.


أَمْ نَجْعَلُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ كَالْمُفْسِدِينَ فِي الْأَرْضِ أَمْ نَجْعَلُ الْمُتَّقِينَ كَالْفُجَّارِ﴿٢٨﴾
28. Je, Tuwajaalie wale walioamini na wakatenda mema kama mafisadi katika ardhi? Au Tuwajaalie wenye taqwa kama waovu?

كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ مُبَارَكٌ لِّيَدَّبَّرُوا آيَاتِهِ وَلِيَتَذَكَّرَ أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿٢٩﴾
29. Kitabu Tumekiteremsha kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) chenye Baraka, ili wapate kuzingatia kwa makini Aayaat zake, na ili wapate kukumbuka wenye akili.


وَوَهَبْنَا لِدَاوُودَ سُلَيْمَانَ ۚ نِعْمَ الْعَبْدُ ۖ إِنَّهُ أَوَّابٌ ﴿٣٠﴾
30. Na Daawuwd Takamtunuku Sulaymaan; uzuri ulioje wa mja! Hakika yeye ni mwingi wa kurudiarudia kutubia.

إِذْ عُرِضَ عَلَيْهِ بِالْعَشِيِّ الصَّافِنَاتُ الْجِيَادُ ﴿٣١﴾
31. Alipohudhurishiwa jioni farasi waliofugwa vyema kabisa wasimamao kidete tayari kukimbia kwa kasi.


فَقَالَ إِنِّي أَحْبَبْتُ حُبَّ الْخَيْرِ عَن ذِكْرِ رَبِّي حَتَّىٰ تَوَارَتْ بِالْحِجَابِ ﴿٣٢﴾
32. Akasema: “Hakika mimi nilipendelea mapenzi ya vitu vizuri badala ya kumdhukuru Rabb wangu mpaka (jua) likatoweka katika pazia (la kiza).” 


رُدُّوهَا عَلَيَّ ۖ فَطَفِقَ مَسْحًا بِالسُّوقِ وَالْأَعْنَاقِ ﴿٣٣﴾
33. (Akasema) “Warudisheni kwangu!” Akaanza kuwapapasa miguu na shingo.


وَلَقَدْ فَتَنَّا سُلَيْمَانَ وَأَلْقَيْنَا عَلَىٰ كُرْسِيِّهِ جَسَدًا ثُمَّ أَنَابَ ﴿٣٤﴾
34. Na kwa yakini Tulimtia mtihanini Sulaymaan, na Tukamtupia juu ya kiti chake mwili kisha akarejea kutubia.


قَالَ رَبِّ اغْفِرْ لِي وَهَبْ لِي مُلْكًا لَّا يَنبَغِي لِأَحَدٍ مِّن بَعْدِي ۖ إِنَّكَ أَنتَ الْوَهَّابُ ﴿٣٥﴾
35. Akasema: “Rabb wangu! Nighufurie, na Nitunukie ufalme asiupate mtu yeyote baada yangu; hakika Wewe Ndiye Mwingi Wa kutunuku.


فَسَخَّرْنَا لَهُ الرِّيحَ تَجْرِي بِأَمْرِهِ رُخَاءً حَيْثُ أَصَابَ ﴿٣٦﴾
36. Basi Tukamtiishia upepo unaokwenda kwa amri yake pole pole popote anapotaka kufika.


وَالشَّيَاطِينَ كُلَّ بَنَّاءٍ وَغَوَّاصٍ ﴿٣٧﴾
37. Na mashaytwaan, kila ajengaye na mpiga mbizi.


وَآخَرِينَ مُقَرَّنِينَ فِي الْأَصْفَادِ ﴿٣٨﴾
38. Na wengineo, wafungwao minyororoni.


هَـٰذَا عَطَاؤُنَا فَامْنُنْ أَوْ أَمْسِكْ بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴿٣٩﴾
39. (Tukasema) “Hiki ni kipawa Chetu, basi toa au zuia bila ya hesabu.”


وَإِنَّ لَهُ عِندَنَا لَزُلْفَىٰ وَحُسْنَ مَآبٍ ﴿٤٠﴾
40. Na hakika yeye bila shaka ana makurubisho Kwetu na marejeo mazuri.  


وَاذْكُرْ عَبْدَنَا أَيُّوبَ إِذْ نَادَىٰ رَبَّهُ أَنِّي مَسَّنِيَ الشَّيْطَانُ بِنُصْبٍ وَعَذَابٍ ﴿٤١﴾
41. Na mkumbuke mja Wetu Ayyuwb alipomwita Rabb wake: “Hakika mimi amenigusa shaytwaan kwa tabu na adhabu.”


ارْكُضْ بِرِجْلِكَ ۖ هَـٰذَا مُغْتَسَلٌ بَارِدٌ وَشَرَابٌ ﴿٤٢﴾
42. (Akaambiwa): “Piga piga ardhi kwa mguu wako!  Hii (chemchemu); maji baridi ya kuogea na ya kunywa.”


وَوَهَبْنَا لَهُ أَهْلَهُ وَمِثْلَهُم مَّعَهُمْ رَحْمَةً مِّنَّا وَذِكْرَىٰ لِأُولِي الْأَلْبَابِ ﴿٤٣﴾
43. Na Tukamtunukia ahli zake na wengine mfano wao pamoja nao ni rahmah kutoka Kwetu, na ni ukumbusho kwa wenye akili.


وَخُذْ بِيَدِكَ ضِغْثًا فَاضْرِب بِّهِ وَلَا تَحْنَثْ ۗ إِنَّا وَجَدْنَاهُ صَابِرًا ۚ نِّعْمَ الْعَبْدُ ۖ إِنَّهُ أَوَّابٌ ﴿٤٤﴾
44. Na (akaambiwa): “Chukua mkononi mwako kicha cha vijiti na upigie navyo na wala usivunje kiapo.” Hakika sisi Tulimkuta mwenye subira mno, uzuri ulioje wa mja, hakika yeye ni mwingi wa kurudiarudia kutubia.


وَاذْكُرْ عِبَادَنَا إِبْرَاهِيمَ وَإِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ أُولِي الْأَيْدِي وَالْأَبْصَارِ ﴿٤٥﴾
45. Na wakumbuke waja Wetu; Ibraahiym, na Is-haaq, na Ya’quwb, wenye nguvu na busara.


إِنَّا أَخْلَصْنَاهُم بِخَالِصَةٍ ذِكْرَى الدَّارِ ﴿٤٦﴾
46. Hakika Sisi Tumewakhitari kutokana na ikhlasi zao kwa kuwapa sifa khalisi ya ukumbusho wa Aakhirah.


وَإِنَّهُمْ عِندَنَا لَمِنَ الْمُصْطَفَيْنَ الْأَخْيَارِ ﴿٤٧﴾
47. Na hakika wao Kwetu bila shaka ni miongoni mwa waliokhitariwa na walio bora kabisa.


وَاذْكُرْ إِسْمَاعِيلَ وَالْيَسَعَ وَذَا الْكِفْلِ ۖ وَكُلٌّ مِّنَ الْأَخْيَارِ ﴿٤٨﴾
48. Na wakumbuke Ismaaiyl na Alyasa’ na Dhal-Kifli, na wote miongoni mwa walio bora kabisa.


هَـٰذَا ذِكْرٌ ۚ وَإِنَّ لِلْمُتَّقِينَ لَحُسْنَ مَآبٍ ﴿٤٩﴾
49. Huu ni ukumbusho, na hakika wenye taqwa bila shaka wana mahali pazuri kabisa pa kurejea.


جَنَّاتِ عَدْنٍ مُّفَتَّحَةً لَّهُمُ الْأَبْوَابُ ﴿٥٠﴾
50. Jannaat za kudumu milele, zitakazofunguliwa milango kwa ajili yao.


مُتَّكِئِينَ فِيهَا يَدْعُونَ فِيهَا بِفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ وَشَرَابٍ ﴿٥١﴾
51. Wakiegemea humo, wakiomba humo matunda mengi na vinywaji.


وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ أَتْرَابٌ ﴿٥٢﴾
52. Na pamoja nao wanawake wenye staha wanaoinamisha macho wa hirimu moja.


هَـٰذَا مَا تُوعَدُونَ لِيَوْمِ الْحِسَابِ ﴿٥٣﴾
53. Haya ndio yale mliyoahidiwa Siku ya hesabu.


إِنَّ هَـٰذَا لَرِزْقُنَا مَا لَهُ مِن نَّفَادٍ ﴿٥٤﴾
54. Hakika hii bila shaka ni riziki Yetu, haina kumalizika.


هَـٰذَا ۚ وَإِنَّ لِلطَّاغِينَ لَشَرَّ مَآبٍ ﴿٥٥﴾
55. Ndio hivi! Na hakika wenye kupinduka mipaka kuasi bila shaka wana mahali pabaya mno pa kurejea.


جَهَنَّمَ يَصْلَوْنَهَا فَبِئْسَ الْمِهَادُ ﴿٥٦﴾
56. Jahannam wataingia kuungua, basi pabaya palioje mahali pa kupumzikia.


هَـٰذَا فَلْيَذُوقُوهُ حَمِيمٌ وَغَسَّاقٌ ﴿٥٧﴾
57. Ndio hivi! Basi wayaonje maji yachemkayo na usaha.


وَآخَرُ مِن شَكْلِهِ أَزْوَاجٌ ﴿٥٨﴾
58. Na (adhabu) nyinginezo za mfano wake na aina yake. 


هَـٰذَا فَوْجٌ مُّقْتَحِمٌ مَّعَكُمْ ۖ لَا مَرْحَبًا بِهِمْ ۚ إِنَّهُمْ صَالُو النَّارِ ﴿٥٩﴾
59.  (Wataambizana): “Hili ndilo kundi litakalotumbukia pamoja nanyi. Hawana makaribisho mazuri. Hakika wao wataingia kuungua motoni.”


قَالُوا بَلْ أَنتُمْ لَا مَرْحَبًا بِكُمْ ۖ أَنتُمْ قَدَّمْتُمُوهُ لَنَا ۖ فَبِئْسَ الْقَرَارُ ﴿٦٠﴾
60. (Waliofuata wapotofu) Watasema: “Bali nyinyi hakuna makaribisho mazuri kwenu!  Nyinyi ndio mliotutangulizia haya basi ubaya ulioje makazi ya kustakiri.”


قَالُوا رَبَّنَا مَن قَدَّمَ لَنَا هَـٰذَا فَزِدْهُ عَذَابًا ضِعْفًا فِي النَّارِ ﴿٦١﴾
61. Watasema: “Ee Rabb wetu! Yule aliyetutangulizia haya basi mzidishie adhabu maradufu katika moto.”


وَقَالُوا مَا لَنَا لَا نَرَىٰ رِجَالًا كُنَّا نَعُدُّهُم مِّنَ الْأَشْرَارِ ﴿٦٢﴾
62. Na watasema: “Tuna nini! Mbona hatuwaoni watu tuliokuwa tukiwahesabu kuwa ni miongoni mwa waovu?”


أَتَّخَذْنَاهُمْ سِخْرِيًّا أَمْ زَاغَتْ عَنْهُمُ الْأَبْصَارُ ﴿٦٣﴾
63. “Je, tuliwafanyia masikhara au yamepotea tu macho yetu?


إِنَّ ذَٰلِكَ لَحَقٌّ تَخَاصُمُ أَهْلِ النَّارِ ﴿٦٤﴾
64. Hakika hayo bila shaka ni kweli; makhasimiano ya watu wa motoni.


قُلْ إِنَّمَا أَنَا مُنذِرٌ ۖ وَمَا مِنْ إِلَـٰهٍ إِلَّا اللَّـهُ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ ﴿٦٥﴾
65. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hakuna Muabudiwa wa haki yeyote isipokuwa Allaah Mmoja Pekee, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika.


رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا الْعَزِيزُ الْغَفَّارُ ﴿٦٦﴾
66. Rabb wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwingi wa kughufuria.


قُلْ هُوَ نَبَأٌ عَظِيمٌ ﴿٦٧﴾
67. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hii (Qur-aan) ni habari muhimu adhimu.


أَنتُمْ عَنْهُ مُعْرِضُونَ ﴿٦٨﴾
68. “Nyinyi mnaikengeuka.


مَا كَانَ لِيَ مِنْ عِلْمٍ بِالْمَلَإِ الْأَعْلَىٰ إِذْ يَخْتَصِمُونَ ﴿٦٩﴾
69. “Sikuwa mimi na elimu yoyote kuhusu wakuu watukufu (Malaika) wanapokhasimiana na kujadiliana.


إِن يُوحَىٰ إِلَيَّ إِلَّا أَنَّمَا أَنَا نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿٧٠﴾
70. “Haifunuliwi Wahy kwangu isipokuwa ya kwamba: hakika mimi ni mwonyaji bayana.”


إِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَائِكَةِ إِنِّي خَالِقٌ بَشَرًا مِّن طِينٍ ﴿٧١﴾
71. Pale Rabb wako Alipowaambia Malaika: “Hakika Mimi Namuumba mtu kutokana na udongo.


فَإِذَا سَوَّيْتُهُ وَنَفَخْتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُوا لَهُ سَاجِدِينَ ﴿٧٢﴾
72. “Basi Nitakapomsawazisha na Nikampuliza humo roho Niliyoiumba; basi mwangukieni kumsujudia.”


فَسَجَدَ الْمَلَائِكَةُ كُلُّهُمْ أَجْمَعُونَ ﴿٧٣﴾
73. Wakamsujudia Malaika wote pamoja.


إِلَّا إِبْلِيسَ اسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ ﴿٧٤﴾
74. Isipokuwa Ibliys, alitakabari na akawa miongoni mwa makafiri.


قَالَ يَا إِبْلِيسُ مَا مَنَعَكَ أَن تَسْجُدَ لِمَا خَلَقْتُ بِيَدَيَّ ۖ أَسْتَكْبَرْتَ أَمْ كُنتَ مِنَ الْعَالِينَ ﴿٧٥﴾
75. (Allaah) Akasema: “Ee Ibliys! Nini kilichokuzuia usimsujudie Niliyemuumba kwa Mikono Yangu? Je, umetakabari, au umekuwa miongoni mwa waliojitukuza?”


قَالَ أَنَا خَيْرٌ مِّنْهُ ۖ خَلَقْتَنِي مِن نَّارٍ وَخَلَقْتَهُ مِن طِينٍ ﴿٧٦﴾
76. (Ibliys) akasema: “Mimi ni bora kuliko yeye, Umeniumba kutokana na moto, naye Umemuumba kutokana na udongo.”


قَالَ فَاخْرُجْ مِنْهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٌ ﴿٧٧﴾
77. (Allaah) Akasema: “Basi toka humo, kwani hakika wewe umetokomezwa mbali na kulaaniwa.


وَإِنَّ عَلَيْكَ لَعْنَتِي إِلَىٰ يَوْمِ الدِّينِ ﴿٧٨﴾
78. “Na hakika laana Yangu iko juu yako mpaka Siku ya malipo.”


قَالَ رَبِّ فَأَنظِرْنِي إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ ﴿٧٩﴾
79. (Ibliys) Akasema: “Rabb wangu! Nipe muhula mpaka siku watakayofufuliwa.”


قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ الْمُنظَرِينَ ﴿٨٠﴾
80. (Allaah) Akasema: “Hakika wewe ni miongoni mwa waliopewa muhula.


إِلَىٰ يَوْمِ الْوَقْتِ الْمَعْلُومِ ﴿٨١﴾
81. “Mpaka siku ya wakati maalumu.”


قَالَ فَبِعِزَّتِكَ لَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ ﴿٨٢﴾
82. (Ibliys) Akasema: “Naapa kwa Utukufu Wako, bila shaka nitawapotosha wote.


إِلَّا عِبَادَكَ مِنْهُمُ الْمُخْلَصِينَ ﴿٨٣﴾
83. “Isipokuwa waja Wako miongoni mwao waliokhitariwa kwa ikhlasi zao.”


قَالَ فَالْحَقُّ وَالْحَقَّ أَقُولُ ﴿٨٤﴾
84. (Allaah) Akasema: “Basi haki ni… Na haki Nasema!


لَأَمْلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكَ وَمِمَّن تَبِعَكَ مِنْهُمْ أَجْمَعِينَ ﴿٨٥﴾
85. “Bila shaka Nitaijaza Jahannam kwa wewe na wote waliokufuata miongoni mwao.”


قُلْ مَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ وَمَا أَنَا مِنَ الْمُتَكَلِّفِينَ ﴿٨٦﴾
86. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Sikuombeni ujira wowote juu ya hili, na wala mimi si miongoni mwa wenye kujidai kuzusha chochote kisichohusu.


إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ ﴿٨٧﴾
87. “Haikuwa hii (Qur-aan) isipokuwa ni ukumbusho tu kwa walimwengu.


وَلَتَعْلَمُنَّ نَبَأَهُ بَعْدَ حِينٍ ﴿٨٨﴾
88. “Na bila shaka mtakuja kujua habari zake baada ya muda.”




Tags

advertisement centil

This blog is created for your interest and in our interest as well as a website and social media sharing info Interest and Other Entertainment.